Events  Activities  ZLSC Community  News  Contact Us
 

NEWS ALERT! Maadhimisho ya siku ya adhabu ya kifo na uzinduzi wa vitabu vya sheria.

 

KITUO CHA HUDUMA NA SHERIA YAZINDUA VITABU VIWILI (2) VYA SHERIA

 

 

 

Kituo cha Huduma na Sheria Zanzibar (ZLSC) leo tarehe 10/10/2011 kimeadhimisha siku ya Adhabu ya kifo   na kuzindua vitabu viwili (2) vya Sheria. 

 

Mgeni rasmi katika kuadhimisha siku ya Adhabu ya kifo na uzinduzi wa vitabu hivyo alikuwa Makamo wa Pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi. 

 

 

 

Ujumbe (theme) wa mwaka huu wa kuadhimisha siku ya Adhabu ya kifo ulikuwa unyama wa Adhabu ya kifo (The humanity of Death Penalty). 

Vitabu viwili vilivyozinduliwa ni Adhabu ya Kifo katika Sheria za Kiislamu (Death Penalty in Islamic Law) kilichotungwa na Dk. Muhyiddin Ahmad Khamis (Maalim Siasa). 

 

Kitabu cha pili ni Zanzibar; The Development of the Constitution, kilichohaririwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya ZLSC, Profesa Chris Maina Peter na Wakili wa Canada Immi Sikand

 

Uzinduzi wa vitabu   hivi viwili kumeongeza idadi ya vitabu vilivyochapishwa na ZLSC  kuwa ni kumi na sita (16). 

 

Maudhui ya kitabu cha Adhabu ya Kifo katika Sheria za Kiislamu ni Adhabu ya Kifo katika nidhamu ya Uislamu ni nyenzo katika nyenzo ambazo zinategemewa katika kuhifadhi jamii kuepukana na kukengeuka na uovu na kwa ajili ya kutia adabu mkosaji. 

 

Aidha, maudhui ya kitabu cha, Zanzibar; The Development of the Constitution kinachoelezea historia ya maendeleo ya Katiba Zanzibar na marekebisho ya kumi ya 2010 Katiba ya Zanzibar yaliyopelekea kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa (GNU) Zanzibar